Wakili niko langoni, leyo tena nimefika

Siji nayo burudani, machozi yatiririka

Naomba nisikieni, nieleze yalotufika

Mola amlaze pema, Walibora katuaga


Hatari barabarani, furaha tena hatuna

Utovu huku mijini, imekua nyingi sana

Dereva bila leseni, mijini mejazana

Mola amlaze pema, Walibora katuaga


Kilio changu cha haki, zumbukuku kanishika

Kifo nitakusitaki, uzoefu sitotaka

Uchungu katamalaki, nitasema nikitaka

Mola amlaze pema, Walibora katuaga


Mashairi katutungia, ugwiji umesheheni

Riwaya katuandikia, isomwe humu shuleni

Studioni kaingia, mhafidhina makini

Mola amlaze pema , Walibora katuaga

Wenzangu nawaeleza , yalotupata jamani

Saa kumi ikianza , ni nyakati za jioni

Walibora aliweza , kutuaga buriani

Mola amlaze pema , Walibora katuaga


Wanafunzi sikieni , penye nia pana njia

Masomo zingatieni , ulegevu kufifia

Usingizi sitieni , vitabuni kipitia

Mola amlaze pema , Walibora katuaga


Wasikizi kwaherini , nimefika ukingoni

Watakao aniwani , wakili mie nyumbani

Nilosema kumbukeni , mkifika majumbani

Mola amlaze pema , Walibora katuaga

By Samson Odhiambo

About Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *